Wednesday 17 December 2014

#‎TANZIA‬ AISHA MADINDA AFARIKI DUNIA!


 
Aliyekuwa mnenguaji wa bendi tofauti hapa nchini Tanzania Aisha Madinda afariki dunia na mwili wake wakutwa umehifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala.



Akiongea na EATV Mkurugenzi wa bendi ya Twanga Pepeta amesema kuwa alipewa taarifa na Daktari mmoja kuwa wameona kama mwili wa Aisha Madinda hospitalini hapo, ndipo akatuma watu kwenda kuangalia akiwemo Luiza Mbutu ili kuhakikisha kama kweli ni yeye ndipo walipogundua ni yeye.


“ Mimi nipo njiani natoka Kigoma kuja Dar es Salaam, ni habari ya kusikitisha sana maana Aisha amefariki katika mazingira ya kutatanisha sana, jana alikuwa mzima na anachati na watu kwenye simu leo napigiwa simu mwili wake umekutwa umehifadhiwa kwenye hospitali ya Mwananyamala, hata sielewi nini kimetokea”. Amesema Asha Baraka

Mungu ailaze roho ya Marehemu Aisha Madinda mahali pema peponi , Amina.


Chanzo:EATV.

No comments:

Post a Comment